Mgodi mkubwa zaidi wa almasi nchini Lesotho, Letšeng, umewafuta kazi wafanyakazi 240, ikiwa ni sawa na asilimia 20 ya wafanyakazi wake, huku ukipambana na bei ya chini ya vito kutokana na mahitaji duni na hali ya kutokuwa na uhakika kuhusu mazingira ya uchumi duniani.
Hii ni kwa mujibu wa kampuni ambayo ndiyo mzalishaji mkuu Gem Diamonds (GEMD.L).
Almasi ni muhimu kwa uchumi wa Lesotho, na sekta hiyo inachangia hadi asilimia 10 ya Pato la Taifa na kutoa ajira kwa maelfu katika nchi yenye watu zaidi ya milioni 2.
Almasi pia ni bidhaa kuu inayouzwa njje ya Lesotho, pamoja na nguo.
Gem Diamonds ilisema mgodi wake wa Letšeng, ambao unazalisha baadhi ya vito vikubwa na vya thamani zaidi duniani kama vile “Lesotho Legend” yenye karati 910, umerekebisha mpango wake wa mgodi na kupunguza ajira ili kupunguza gharama.
“Shinikizo la bei endelevu, mahitaji muhimu katika masoko, kutokuwa na uhakika unaoendelea wa uchumi na siasa za dunia, pamoja na kutokuwa na uhakika wa ushuru kwa India, yote haya yanafanya hali kuwa ngumu kwa biashara,” Mkurugenzi Mtendaji wa Gem Diamonds Clifford Elphick alisema katika taarifa.