Mwanasheria Mkuu wa Uganda anasisitiza kuwa nchi hiyo imejitolea kwa makubaliano na Marekani kupokea watu waliofukuzwa kutoka nchi hiyo.
Hayo yamethibitishwa Agosti, 2025.Hata hivyo, Uganda inasema makubaliano hayo yana masharti.
Kwa mfano Uganda imesema mpango huu ni wa muda na kwamba haitakubali kupokea watu walio na historia ya uhalifu na watoto ambao hawajaandamana na wazazi wao hawatakubaliwa.
Uganda pia imependekeza kupokea watu kutoka nchi za Kiafrika.Lakini ni lipo lengo la Uganda la kukubali makubaliano hayo?
Uganda sasa inakuwa nchi ya nne kuwapokea wananchi waliofukuzwa Marekani baada ya Rwanda, Sudan Kusini na Eswatini.
Nchi nyingine, ikiwa ni pamoja na Eswatini, zimeripotiwa kukubali mpango huo ili kuondolewa ushuru iliyowekewa na Marekani.
Nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika ambayo inauza nguo, matunda, karanga na sukari mbichi kwenda Marekani ilipigwa ushuru wa asilimia 10 na Marekani.
Mpaka kusikia mwezi Julai mwaka huu, tayari ilikuwa imepotea watu watano.Rwanda nayo imethibitisha kuwa itachukua watu 250 ingawa tarehe rasmi haijatajwa.