Miaka michache iliyopita, Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) kilikuwa na sura ya Mzee Hashim Spunda Rungwe na sera yake maarufu ya ‘ubwabwa kwa wote.’

Ilikuwa ni kawaida kumuona mzee huyo, ambaye ndie muasisi wa chama hicho akiwa amezungukwa na watu wachache kwenye kampeni zake na baadaye ‘kujichana’ wali, maharage na nyama baada ya mikutano ya kampeni.

Ila kwa sasa, mambo yamebadilika. Hasa baada ya kundi kubwa la waliokuwa wanachama na viongozi wa Chadema kuhamia Chaumma.

Hivi sasa Salum Mwalim ndiye sura halisi ya chama hicho kilichoanzishwa mwaka 2013.

Mwalim, ambaye ni mwandishi wa habari kitaluuma, ndie anayepeperusha bendera ya chama hicho kwa nafasi ya urais, kwa upande wa Tanzania Bara, huku akisindikizwa na Devotha Minja, ambaye pia ni mwanahabari, akiwa mgombea mwenza wake.

Itakumbukwa kuwa, Salum Mwalim alikuwa ni miongoni wa watu waliokihama chama cha CHADEMA, wakidai kutofurahishwa na mwenendo wa uongozi mpya wa chama chini ya Mwenyekiti wa wa sasa, Tundu Lissu, ambae anakabiliwa na kesi ya uhaini pamoja na makosa mengine.

Wengine waliokihama chama hicho ni pamoja na Benson Kigaila, John Mrema na Devotha Minja.

Ndani ya CHADEMA, Salum Mwalim alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ile ya unaibu katibu Mkuu kwa upande wa Zanzibar.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *