Wizara ya Ulinzi ya Uturuki imekana ripoti ya kwamba Israel ililenga vifaa vya Vikosi vya Kijeshi vya Uturuki nchini Syria, ikisisitiza kuwa madai hayo “hayana ukweli wowote.”
Katika taarifa iliyotolewa Alhamisi, wizara hiyo ilielekeza macho yake kwenye shambulio la Israel nchini Qatar, ikisema hili ni ushahidi kwamba Tel Aviv imefanya ugaidi kuwa “sera ya taifa, inayochochea mizozo na kupinga amani.”
Ankara ilieleza kuwa shambulio hilo lilikuwa “ukiukaji mkubwa wa uhuru wa Qatar” na kutangaza: “Tunasimama kidete na Qatar dhidi ya shambulio hili.”
“Mashambulio yasiyo na mipaka”