Mripuko wa ugonjwa huo hatari uliripotiwa mapema mwezi huu kwenye kitongoji cha Bulape na kusababisha vifo vya watu 16 na wengine 68 wanashukiwa kuwa wameambukizwa.

WHO imesema dozi za awali zipatazo 400 za chanjo aina ya Ervebo zimetolewa na shehena nyingine ya chanjo itapelekwa siku chache zinazokuja.

Miongoni mwa wanaopatiwa chanjo hizo ni maafisa wa afya walio mstari wa mbele na watu wanaoaminika huenda watapata maambukizi kutokana na ukaribu wao na waliokwishaambukizwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *