Siku ya Kimataifa ya Demokrasia: Mambo yakoje nchini Uganda?Siku ya Kimataifa ya Demokrasia: Mambo yakoje nchini Uganda?

Mienendo ya kamatakamata ya wafuasi wa vyama vya upinzani na hasa kuelekea kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu, ni miongoni mwa vielelezo vya kudorora kwa demokrasia nchini Uganda.

Wadadisi wa kisiasa na viongozi wa kisiasa wanakosoa kuanzia taasisi za kijeshi, sheria na bunge kwa kuhusika katika vitendo hivyo vinavyokiuka si tu haki za binadamu lakini dhana na falsafa ya demokrasia.

Katika kipindi cha wiki tatu hivi viongozi na wafuasi kadhaa wa upinzani walikamatwa kwa kiviziwa na askari waliovalia kiraia ambao waliwaburuta na kuwasukumia kwenye magari ya kiraia na kuwapeleka mahali pasipokujulikana.

Jeshi la Polisi lakana kamatakamata ya kiholela

Uganda Kampala 2024 | Vikosi vya usalama vikilinda makao makuu ya chama cha kiongozi wa upinzani Bobi Wine
Polisi wakiwa wameizingira ofisi ya chama cha upinzani nchini Uganda, NUP kinachoongozwa na Robert Kyagulanyi, Julai 22, 2024Picha: Abubaker Lubowa/REUTERS

Msemaji wa idara ya mawasiliano ya jeshi, Brigedia Jenerali Felix Kulayigye amesema watu hao hawakutekwa nyara kama inavyodaiwa, ila walikamatwa kisheria wakihusishwa na tuhuma mbalimbali na hufikishwa mahakamani.

Amefahamisha kuwa wafuasi na viongozi wa chama cha upinzani cha NUP wamekamatwa hivi karibuni baada ya kuandaa gwaride la kijeshi kuadhimisha siku ya kuzaliwa rais wa chama hicho Robert Kyagulanyi al maarufu Bobi Wine.

Wadadisi wanasema ingawa uchaguzi huchukuliwa kuwa msingi wa demokrasia, hali ni tofauti kabisa pale vyama vya upinzani vinapozuiwa kuendesha shughuli zake pamoja viongozi wao kukamatwa na kuendelea kuzuiliwa huku kesi dhidi zao zikiendeshwa kwa hali ya kuwavunja moyo. 

Besigye afikishwa mahakama ya kijeshi

To view this video please enable JavaScript, and consider upgrading to a web browser that supports HTML5 video

Kiongozi wa chama cha upinzani PFF, Dkt Kizza Besigye amendelea kubaki gerezani licha ya kuwa na haki ya dhamana. Kwa mtazamo wao, hakuna haja ya uchaguzi kufanyika kama demokrasia halisi hata ndani ya vyama vyenyewe haina uhalisia. 

Huku siku hii ya kimataifa ya demokrasia ikiadhimishwa tarehe 15 Septemba, tarehe 12 ni siku ambayo wanasiasa Uganda wameiweka kuwa kumbukumbu ya siku ambapo  bunge la Uganda liliondoa ukomo wa umri kwa mgombea urais kwemye katiba na hivyo kumwezesha Rais Yoweri Museveni kuendelea kugombea na kutawala.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *