Umoja wa Mataifa unawashutumu viongozi tawala wa Sudan Kusini kwa kujihusisha na uporaji wa kweli wa rasilimali ya mafuta ya nchi hiyo. Ripoti hii ya Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu inaeleza jinsi mapato ya mafuta na yasiyo ya mafuta yanavyoelekezwa kupitia mipango isiyoeleweka na ili kukidhi maslahi ya kisiasa, na kuwanyima mamilioni ya Wasudan Kusini huduma za kimsingi.
