Ushindi huu wa Algeria unawafanya kuwa na jumla ya alama 22 ikiwa bado wamebakisha mechi moja kucheza katika kundi G. Itakuwa fainali ya tano ya Kombe la Dunia lakini ya kwanza tangu mashindano yaliyochezwa Brazil 2014.

Timu itakayoibuka wa kwanza katika kila kundi kwa makundi tisa ya Afrika inafuzu moja kwa moja kwa mashindano hayo yatakayochezwa Canada, Mexico na Marekani, na Algeria inaungana na Morocco, Tunisia na Misri ambao pia tayari wamefuzu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *