Hata hivyo, Trump hakubainisha iwapo kuachiliwa huko kutajumuisha miili ya mateka waliofariki dunia.
Awali Trump alitangaza kuwa Israel na Hamas wametia saini katika awamu ya kwanza ya makubaliano ya Gaza yaliyopendekezwa na Marekani.
Mpango huo wenye vipengele 20, uliotangazwa kwa mara ya kwanza tarehe 29 Septemba, unajumuisha kuachiliwa kwa mateka wote wa Israel kwa kubadilishana na wafungwa wa Kipalestina, kusitishwa kwa mapigano, kupokonywa silaha kwa Hamas, na kuijenga upya Gaza.
Tangu Oktoba 2023, mashambulizi ya Israel yameua takriban Wapalestina 67,200 katika eneo hilo, wengi wao wakiwa wanawake na watoto.
Mashambulio hayo ya mara kwa mara yameifanya Gaza kuwa bila watu, na kusababisha njaa na magonjwa.