Kuanzia Oktoba 23, nchi hiyo ya Afrika Mashariki itakuwa katika kundi la nchi saba za Afrika, ambazo raia wake watatakiwa kulipa dhamana itakayorudishwa ya kati ya dola 5,000, sawa na shilingi milioni 12 za Tanzania au dola 15,000 ambazo ni sawa na shilingi milioni 37.

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, agizo hilo linawahusu wale watakaoomba viza kwa ajili ya biashara B-1 (Business) na utalii B-2 (Tourism).

Serikali ya Marekani imesema agizo hilo linafuatia taarifa za baadhi ya raia kutoka mataifa hayo kupitiliza muda wao pindi wanapokuwa nchini Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *