Katika ziara hiyo ya kampeni katika Jimbo la Tumbatu Kaskazini Unguja Othman alisikiliza kero za wananchi ikiwa ni pamoja na hofu ya kuhamishwa katika eneo hilo ili kupisha ujenzi wa soko.

Kwa upande wake, mgombea urais huyo wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, amesema kuwa sera ya chama chake ni kuhakikisha kwamba Wazanzibar wanasaidiwa, vifaa, elimu na kuwezeshwa kuzalisha kwa tija kwenye sekta mbali mbali ikiwemo ya uvuvi ili kuweza kuuza samaki na mazao mengine ya bahari ndani na nje ya nchi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *