Thamani ya dhahabu yake hata hivyo bado imekadiriwa kwa viwango vya tangu mwaka 1973, ikiweka thamani yake takriban dola bilioni kumi na mja.
Kwa hiyo iwapo serikali ya Marekani itaamua kufanya makadirio mapya ya thamani ya dhahabu yake, huenda ikazidi dola trilioni moja yaani itakuwa zaidi ya asili mia tisini ya thamani yake ya ujazo.
Iwapo hili litafanyika, kuna uwezekano kuwa hifadhi za Marekani za dhahabu zikamudu kulipa takriban nusu ya deni lake.
Haitakuwa mara ya kwanza kwa nchi kufanyia makadirio mapya ya thamani yake ya dhahabu, kwani ishafanyika Ujerumani, Afrika Kusini na Italia, ambapo iliwawezesha kulipa madeni yao ya nje.
Tishio kwa thamani ya sarafu ya Dola
Changamoto ya Marekani kufuata mkondo huu, ni kuwa itasukuma zaidi ukosefu wa imani kimataifa kwa sarafu ya dola ya Marekani kama mdhamini.
Hii ikimaanisha thamani ya dola kimataifa itaanguka. Hii pia itasababisha nchi zaidi kufuata mkondo kama huu, na hivyo kusukuma thamani ya dhahabu juu kupita kiasi.
Ndio ni njia mojawapo ya Marekani kujikwamua kutoka deni kubwa la nje. Lakini kumbuka kushusha thamani ya dola ina hatari kubwa ndani ya Marekani kwani inaweza kuwa sababu ya serikali kukosa umaarufu kutokana na hasira za wananchi.
Kwa hiyo hatua za Trump kuhusu dhahabu ya Marekani inasubiriwa na wengi.Lakini wakati wanasubiri, kama tulivyotaja awali, benki kuu za dunia zimeanza kununua na kuhodhi dhahabu kwa kiasi kikubwa kama sehemu ya tahadhari.