Akizungumza katika Mkutano wa 5 wa Biashara na Uchumi kati ya Uturuki na Afrika uliofanyika Alhamisi jijini Istanbul, Bolat alisema mkutano huo umefanyika wakati wa hali ya sintofahamu duniani, sera za kibiashara za kulinda masoko ya ndani, na changamoto kwa mfumo wa biashara wa kimataifa unaozingatia kanuni.

“Tunafurahi kuendeleza uhusiano wetu kwa kina na kimkakati katika nyanja za kiuchumi, biashara, utamaduni na kijamii kati ya Uturuki na nchi zote za bara la Afrika. Tunalenga kuendeleza uhusiano huo kwa misingi ya haki, usawa, utakaofaidisha pande zote, na tutaendelea kutekeleza sera hizi kwa imara zaidi,” alisema Bolat.

Alieleza kuwa jumla ya biashara ya Uturuki na Afrika imeongezeka kwa zaidi ya mara saba tangu mwaka 2003.

“Zaidi ya hayo, wakandarasi wa Kituruki pia wamechangia sana katika maendeleo ya Afrika kwa kushiriki katika miradi ya maendeleo 2,043 katika nchi mbalimbali za Afrika, na kukamilisha kazi za ujenzi zenye thamani ya karibu dola bilioni 100,” aliongeza.

Miradi mikuu

Bolat alisisitiza kuwa Shirika la Ndege la Uturuki, ambalo ndilo linalobeba bendera ya Uturuki, linaunganisha Afrika na dunia nzima kupitia Istanbul, kwa safari za ndege hadi vituo 62 katika zaidi ya nchi 40 za Afrika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *