Saa kumi na moja jioni kwa saa za Afrika Mashariki, maziko yalikamilika ya hayati Raila Odinga, kiongozi wa muda mrefu wa upinzani nchini Kenya aliyewahi kuhudumu kama Waziri Mkuu wa nchi hiyo.

Raila alizikwa kwa heshima kamili ya kijeshi, huku wanajeshi wakilibeba jeneza lake na kulishusha kaburini.

Viongozi mbali mbali wakiwemo Rais William Ruto, marais wastaafu Uhuru Kenyatta na Olusegun Obasanjo, na waakilishi wengine pamoja na mjane wake Ida Odinga familia, mawaziri magavana na maseneta, pamoja na wageni wengine waheshimiwa walipokezana muda wa kumwaga mchanga kaburini na kuweka maua pembeni mwa kaburi.

Ibada ya wafu iliongozwa na Askofu wa Anglikana wa Siaya, David Kodia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *