
Baadaye wizara ya Ulinzi ya Marekani ilitangaza kuwa ilizishambulia meli kadhaa za Columbia zinazoshukiwa kuhusishwa katika biashara hiyo haramu.
Hayo yanajiri baada ya rais Donald Trump kumtaja Petro kuwa ni mfanyabiashara haramu wa dawa za kulevya huku akimuonya kuchukuwa hatua dhidi ya shughuli hizo kabla ya Marekani kuingilia kati kwa hatua ambazo amesema hazitakuwa nzuri.
Huu ni msuguano wa hivi punde zaidi kati ya Marekani na mmoja wa washirika wake wa karibu katika eneo la Amerika ya Kusini baada ya wiki kadhaa za kurushiana maneno makali. Mwaka 2023, Colombia ilipokea msaada wa dola milioni 740 kutoka Marekani huku nusu ya fedha hizo zikitengewa mamlaka za kukabiliana na biashara ya dawa za kulevya.