Ofisi ya mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini  Yemen , imesema wafanyakazi hao akiwemo mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto UNICEF nchini Yemen, wanazuiliwa katika kituo kilichopo katika kitongoji cha Hada kusini magharibi mwa mji wa Sanaa.

Umoja wa Mataifa umesema unawasiliana na kundi hilo la waasi pamoja na wadau wengine ili kujaribu kutafutia suluhu tatizo hilo na kurejesha udhibiti kamili wa vituo vyake huko Sanaa.

Waasi wa Kihouthi  wamekuwa wakiwashutumu bila ushahidi wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa kuwa majasusi wa Marekani na Israel, shutuma zinazokanushwa na Umoja wa Mataifa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *