Mkutano huo nchini Israel unalenga kujaribu kunusuru mkataba wa usitishaji vita Gaza.

Hii ni baada ya mkataba huo tete kukumbwa na mtihani mkubwa pale Israel iliposema wanamgambo wa Hamas wamewaua wanajeshi wake wawili.

Jeshi la Israel limesema limeanza tena kuhakikisha makubaliano ya usitishaji vita yanatekelezwa na kwamba misaada itaanza kuruhusiwa kuingia Gaza.

Ni zaidi ya wiki moja sasa tangu mkataba wa usitishaji vita kati ya Israel na wanamgambo wa Hamas ulipoanza kutekelezwa.

Tangu mkataba huo ulipoanza, wanamgabo wa Hamas wameingia mitaani na kumetokea makabiliano na magenge mengine yenye silaha.

Awamu inayofuata ya mkataba huo inatarajiwa kuangazia kuipokonya Hamas silaha na kuondoka zaidi kwa vikosi vya Israel katika maeneo mengine ya Gaza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *