Takaichi

Chanzo cha picha, Reuters

Baraza la mawaziri la Waziri mkuu wa Japan Shigeru Ishiba limejiuzulu kuelekea bunge kupiga kura ya kulipeleka taifa hilo kwenye uchaguzi unatorajiwa kumchagua waziri mkuu wa kwanza mwanamke.

Sanae Takaichi anayeongoza chama tawala Liberal Democratic Party hata hivyo ataongoza serikali ya wawakilishi walio wachache.

Mwandishi wa BBC anasema bi Takaichi ni mhafidhina mwenye misimamo mikali asiye na rekodi ya kupigania haki za wanawake.

Wachambuzi Japan wanasema kuchaguliwa kwake ni mkakati wa chama chake kukabiliana na ushawishi unaoshika kasi wa chama cha mrengo wa kulia cha Senseito.

Bi Takaichi anatarajiwa kushughulikia masuala ya mfumko wa bei na ongezeko la gharama ya maisha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *