Uchaguzi mkuu wa Uganda kufanyika Januari 15
Tume ya Uchaguzi ya Uganda imetangaza rasmi kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanyika tarehe 15 Januari. Katika uchaguzi huo, Rais Yoweri Museveni, mwenye umri wa zaidi ya miaka 80, atawania muhula wa saba madarakani.