Makamu Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Gilles Carbonnier ameeleza kuwa kwa sasa, kuna takriban mizozo 50 ya silaha inayoendelea barani humo.

Hiyo inaashiria ongezeko la asilimia 45 tangu mwaka 2020 na hivyo kuiweka mizozo ya Afrika kuwa asilimia 40 ya mizozo yote ya silaha ulimwenguni.

Miongoni mwa nchi zinazozongwa na mizozo ya silaha ni kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Sudan, Mali na Niger

Bara hilo lina takriban watu bilioni 1.4, na lina utajiri wa madini na idadi kubwa ya vijana. Lakini sehemu nyingi ya bara hilo zimekumbwa na umaskini na ukosefu wa usalama.

Kulingana na Carbonnier, mizozo hiyo imesababisha watu milioni 35 kuyakimbia makaazi yao, hiyo ikiwa takriban nusu ya wahamiaji wote ulimwenguni.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *