Marekani imetangaza vikwazo vipya vinavyolenga makampuni mawili makubwa zaidi ya mafuta nchini Urusi – Rosneft na Lukoil – katika juhudi za kuishinikiza Moscow kufanya mazungumzo ya makubaliano ya amani nchini Ukraine.
“Kila wakati ninapozungumza na Vladimir, ninakuwa na mazungumzo mazuri na kisha hawaendi popote,” Rais Donald Trump alisema, baada ya mkutano na Katibu Mkuu wa Nato Mark Rutte kujadili mazungumzo ya amani.
Tangazo la vikwazo hivyo limekuja siku moja baada ya Trump kusema kuwa mkutano uliopangwa kufanyika na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Budapest utasitishwa kwa muda usiojulikana.
Mapema Jumatano, Urusi ilitekeleza mashambulizi makali ya mabomu dhidi ya Ukraine yaliyoua takriban watu saba wakiwemo watoto.
#chanzobbcswahili
#StarTvUpdate