Ruth Chepngetich, mshindi maarufu wa mbio za Chicago Marathon 2024 na mmiliki wa rekodi ya dunia kutoka Kenya, amepigwa marufuku ya miaka mitatu baada ya kubainika kutumia dawa za kuongeza nguvu zilizopigwa marufuku, hydrochlorothiazide (HCTZ).

Sampuli yake ya mkojo iliyochukuliwa mwezi Machi ilionyesha kiwango cha dawa hiyo kilichozidi kiwango kinachoruhusiwa mara 190.

Kitengo cha Uadilifu wa Riadha (AIU) kimethibitisha adhabu hiyo huku ikisisitiza kwamba mafanikio na rekodi zake zote kabla ya Machi 14, 2025 zitaendelea kutambuliwa.

Awali, mwanariadha huyo alikana kabisa kutumia dawa hiyo, akisema “hakuwa na maelezo yoyote kuhusu matokeo ya kipimo hicho”, na akasisitiza kwamba hajawahi kutumia dawa za kuongeza nguvu.

Hata hivyo, baadaye alibadilisha kauli yake, akidai kwamba alikuwa amekunywa dawa za mfanyakazi wake wa nyumbani baada ya kuugua siku mbili kabla ya kipimo hicho — jambo ambalo alisema alishindwa kulieleza kwa wachunguzi wa AIU.

AIU ilisema maelezo hayo mapya “hayaaminiki kabisa.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *