Erdogan alisema kuwa mazungumzo yanaendelea kuhusiana na kuunda kikosi kazi cha kimataifa kitakachoendesha Gaza, na kwamba maelezo zaidi bado yanakamilishwa.

“Ni jambo lenye vipengele vingi, kwa hivyo mazungumzo ya kina yanaendelea,” Erdogan alisema kwa waandishi wa habari alipokuwa kwenye ndege yake Ijumaa, akirejea kutoka ziara zake Kuwait, Qatar na Oman. “Tuko tayari kutoa kila aina ya msaada, na maandalizi yetu yanaendelea.”

Kauli yake inakuja huku Uturuki ikisisitiza juhudi za kimataifa za kudumisha utulivu Gaza na kuhakikisha usitishaji vita uliyo dhaifu yanadumu, huku Israel ikiendelea kuyakiuka.

“Hamas inafuata makubaliano ya kusitisha mapiganoa na imethibitisha kwa uwazi dhamira yake ya kufanya hivyo,” Erdogan ameisema. “Israel, hata hivyo, inaendelea kuyakiuka. Jumuiya ya kimataifa, hasa Marekani, lazima iweke juhudi zaidi kuhakikisha Israel inatii kikamilifu.”

Erdogan alisema kuwa shinikizo la kidiplomasia kwa Israel ni “jambo muhimu,” na kuongeza kuwa vikwazo na kusitisha mauzo ya silaha vinaweza kusaidia kulazimisha Israel kutimiza ahadi zake.

Inayohusiana

Juhudi za Uturuki za misaada wa kibinadamu na kujengwa upya kwa Gaza  

Erdogan ameahidi kuwa Uturuki itaendelea kutoa misaada ya kibinadamu isiyozuiliwa Gaza na kuchukua nafasi muhimu katika ujenzi upya wa eneo hilo lililoharibiwa na vita.

“Gaza itainuka tena — hakuna anayepaswa kutilia shaka hilo,” alisema. “Hatujawahi kuacha kutuma msaada wetu nchini Misri, na tutaendelea kufanya hivyo.”

Alibainisha kuwa Meli ya Wema ya 17 ya Uturuki, iliyobeba misaada ya kibinadamu, hivi karibuni ilifika Bandari ya El-Arish nchini Misri. Mashirika ya serikali ya Uturuki na isiyo ya serikali a, yamejipanga kusaidia kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa Gaza, amesema Erdogan.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *