Sirikit, mama yake Mfalme wa Thailand Vajiralongkorn, alifariki jijini Bangkok. Alikuwa na umri wa miaka 93.

Alifariki akiwa hospitali saa tatu na dakika ishirini na moja siku ya Ijumaa, kulingana na taasisi inayoshughulikia masuala ya Kifalme.

Iliongeza kuwa kundi la madaktari ambalo limekuwa likifuatilia afya yake tangu Septemba 7, 2019, lilimpata akiugua maradhi kadhaa na kutaka awe chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Madaktari wanasema Sirikit alipatikana na matatizo kwenye mfumo wake wa damu Oktoba 17, na licha ya kutibiwa, hali yake ikaendelea kuwa mbaya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *