VIONGOZI wa Afrika wamekusanyika mjini Algiers, Algeria, kuhimiza kuwa uhalifu wa enzi za ukoloni unapaswa kutambulika, kuhalalishwa kama jinai na kushughulikiwa kupitia malipo ya fidia.

Mkutano huo uliwaleta pamoja wanadiplomasia na viongozi wa bara hilo kujadili azimio la Umoja wa Afrika lililopitishwa mapema mwaka huu, linalolenga haki na fidia kwa waathirika wa ukoloni. SOMA: Umoja wa Afrika wampongeza Mutharika kwa ushindi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria, Ahmed Attaf, alisema katika hotuba yake ya ufunguzi kuwa uzoefu wa Algeria chini ya utawala wa Kifaransa unaonyesha umuhimu wa kudai fidia na kurejesha mali iliyoibiwa. Aliongeza kuwa mfumo wa kisheria nchini humo utahakikisha urejeshaji mali hauonekani kama ‘zawadi au upendeleo.’

Attaf pia alibainisha kuwa mkataba wa Umoja wa Mataifa unakataza kunyakua maeneo kwa nguvu, lakini hautaji waziwazi kuhusu ukoloni. Ukosefu wa rejeleo hilo ulikuwa kiini cha kilele cha Umoja wa Afrika mwezi Februari, ambapo viongozi walijadili pendekezo la kuunda msimamo wa pamoja kuhusu fidia na kufafanua ukoloni kamakosa la jinai dhidi ya binadamu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *