Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa China, Lin Jian, amesema matakwa ya China yakiathirika kwa namna yoyote  ile, itachukua hatua sawa kulinda usalama na maslahi yake. Jian amesema tabia ya Marekani ni ya unyanyasaji.

Hata hivyo, wizara ya uchumi ya China ilisema katika taarifa tofauti kwamba inatumai Marekani itakuwa makini katika maneno na matendo yake na kutatua tofauti zake za kibiashara na kiuchumi kupitia mazungumzo.

Awali Trump alivihusisha vikwazo zaidi vya Marekani dhidi ya Urusi kwa mataifa ya NATO akiweka ongezeko la ushuru la asilimia 50 hadi 100 kwa bidhaa za China na kukataa mataifa hayo kununua mafuta ya Urusi. Trump alisema anaamini hatua hiyo itasaidia kuvimaliza vita vya Urusi na Ukraine.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *