Wananchi wa Guinea wanapiga kura ya ndiyo au hapana kuhusu rasimu ya Katiba mpya. Rasimu hiyo inalenga kuchukua nafasi ya katiba ya mpito inayotumika tangu mapinduzi ya Septemba 21, 2021 ambayo yalishuhudia Mamadi Doumbouya akimpindua rais Alpha Condé. Zaidi ya wapiga kura milioni 6.5 kati ya milioni 14.5 nchini humo wanatarajiwa kupiga kura zao. Uchaguzi huu unaashiria hatua muhimu katika mpito kuelekea kurejea kwa utaratibu wa kikatiba.
