Chanzo cha picha, Reuters
Ryan Routh
amepatikana na hatia ya kujaribu kumuua Rais Donald Trump kwenye uwanja wa gofu
wa Florida Septemba mwaka jana.
Mahakama ilimpata
Routh, 59, na hatia ya mashtaka yote, ikiwa ni pamoja na jaribio la mauaji ya
mgombea mkuu wa urais na makosa kadhaa ya kutumia silaha.
Tukio hilo
lilitokea tarehe 15 Septemba 2024 wakati Trump, ambaye wakati huo alikuwa
mgombea urais, alikuwa akicheza gofu kwenye uwanja anaoumilik uliopo katikaufukwe wa West Palm Beach,
takriban dakika 15 kutoka kwa makazi yake ya Mar-a-Lago.
Routh alijaribu kujidhuru baada ya hukumu kusomwa, kulingana na mshirika wa BBC wa Marekani, CBS News. Inasemekana alijaribu kujichoma kisu kwa kutumia kalamu kabla ya Wanajeshi wa Marekani kuingilia kati.
Katika chapisho la mtandao wa kijamii mara baada ya hukumu hiyo, Trump alishukuru vyombo vya sheria na shahidi ambaye alitoa taarifa zilizofanikisha kukamatwa kwa Routh.
Trump alisema kuhusu Routh: “Huyu alikuwa mtu muovu mwenye nia mbaya, na walimkamata. Wakati mkubwa sana kwa HAKI NCHINI AMERIKA!”.
Mwanasheria mkuu wa serikali Pamela Bondi alisema: “Jaribio hili la kumuua halikuwa tu shambulio kwa rais wetu, bali ni dharau kwa taifa letu.”