Dunia inaungana Agosti 30 kuadhimisha siku ya watu waliopotea,takwimu zikisema kuna watu karibu laki tatu ambao hawajulikani waliko, kote ulimwenguni. Baadhi ya watu waliotenganishwa na wapendwa wao ni wakimbizi waliofurushwa makwao kutokana na vita au mizozo tofauti.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Katika kambi ya Kakuma 3  tulikutana  na  Amar Adam mkimbizi kutoka  eneo la Darfur nchini Sudan  ambaye  alitenganishwa na ndugu zake tangu alipokimbia vita mwaka 2004.

Amar Adam mkimbizi kutoka Sudan
Amar Adam mkimbizi kutoka Sudan © Carol Korir

 Kamati ya  kimataifa ya msalaba mwekundu ikishirikiana na Shirika la  msalaba mwekundu nchini ,katika mpango maalum wa kurejesha   na kudumisha uhusiano wa kifamilia ,zimekuwa kwenye mradi wa miaka kujaribu kuwaunganisha wakimbizi hao na wapendwa hao ili kuwapa hao ahueni.

Wafanya kazi wa ICRC wakizungumza na wakimbizi katika kambi ya Kakuma
Wafanya kazi wa ICRC wakizungumza na wakimbizi katika kambi ya Kakuma © ICRC

Kwenye mpango huo,mkimbizi anaweza kuchagua kuandika ujumbe maalum kwa wapendwa wake ambao unatumwa kwa kwa ushirikiano wa ICRC na mashirika ya msalaba mwekundu  katika mataifa husika.

Iwapo atafualu kupata nambari za simu , wahudumu wa shirika la  msalaba mwekundu nchini Kenya wanapa nafasi ya kupiga simu mara moja  kwa mwezi kwa angalau dakika mbili.

Kwa wale ambao wana wanafamilia ambao wana simu za kisasa kuna huduma ya WIFI katika maeneo maalum na kwenye ofisi za Kenya Redcross ambapo wanaunganishwa na kupiga simu kutumia WhatsApp au Facebook ,mfumo ambao ICRC na Kenya Redcross zinasema ni maarufu kwa kuwa wakimbizi hao wanaweza kuonana kwa njia ya video na wapendwa wao.

Kamati ya kimataifa ya msalaba Mwekundu,ICRC na Shirika la Msalaba mwekundu Kenya,KRC, ziko mbio kuwaunganisha wakimbizi waliotenganishwa na familia zao kupitia mpango wa Restoring Family Links
Kamati ya kimataifa ya msalaba Mwekundu,ICRC na Shirika la Msalaba mwekundu Kenya,KRC, ziko mbio kuwaunganisha wakimbizi waliotenganishwa na familia zao kupitia mpango wa Restoring Family Links © Carol Korir

Kupitia mfumo wanapata muda mwingi wa kuzungumza kwa kuwa gharama yake ni ndogo.

Kwa wale ambao hawajafanikiwa  kupata namba ya simu ,huendelea kuwasiliana kwa njia ya ujumbe maalum au barua.

Mary Muteti  kutoka Kenya Red Cross eneo la Kakuma  anasema wakimbizi hao wanapozungumza na wapendwa wao ,wanakuwa watulivu na kuweza kuishi kwa matumaini.

Mary Muteti akiwa na mhudumu mwenzake wa shirika la msalaba mwekundu Kakuma
Mary Muteti akiwa na mhudumu mwenzake wa shirika la msalaba mwekundu Kakuma © Carol Korir

ICRC inasema mwaka jana katika kambi ya Kakuma na Daadab iliweza kufanikisha simu

123, 767 zinazotumia WIFI na kusambaza ujumbe 4,041 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *