g

Chanzo cha picha, Ana Lolenzana

Washindi wa tuzo ya Micheline Masala y Maiz wana matumaini ya kueneza mtindo wao kote Mexico na duniani kote.

Wakati Norma Listman na Saqib Keval, ambao ni wamiliki na wapishi katika mojawapo ya migahawa maarufu ya Mexico City, Masala y Maiz, waliposhinda nyota yao ya kwanza ya Michelin, walikuwa New York City kwenye tafrija ya mpishi mwenzao.

“Timu yetu ilikuwa ikitupigia simu, na hatukuwa tukipokea simu,” anaelezea Listman huku akicheka. “Halafu mmoja wa mameneja wetu mkuu zaidi, ambaye kwa kawaida huwa hapigi simu isipokuwa kama kuna kitu kibaya akapiga simu. Ikabainika kuwa tulikuwa moja kwa moja kwenye jukwaa [kwenye tuzo za Michelin].”

Wanandoa, wanaojulikana kwa kuanzisha mgahawa wa kipekee “Kula Unachotaka, Lipa Unachoweza”, wana shauku ya kusaidia jamii zaidi kuliko kupata sifa za kifahari.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *