Kornelius amesema  katika mazungumzo ya njia ya simu kati ya Merz na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, Ujerumani iliahidi kuendelea kuiunga mkono Kiev na kuimarisha ushirikiano wake wa kiulinzi.

Zelensky ameishukuru Ujerumani kwa kuendelea kuiunga mkono akisema Urusi imetumia droni na makombora kutekeleza shambulizi aliloliita la kigaidi dhidi ya taifa lake lililolenga miundombinu yake ya nishati.

Wakati huo huo Zelensky pia alizungumza kwa njia ya simu na rais wa Marekani Donald Trump leo Jumamosi na kumtaka awezeshe kufikiwa makubaliano ya amani ya Ukraine kama alivyofanya katika eneo la Mashariki ya Kati.

Zelensky amesema kama vita vinaweza kusitishwa katika eneo moja vinaweza pia kusitishwa katika eneo lengine, akimaanisha uhasama kati ya Ukraine na Urusi ulioanza mwaka 2022 baada ya Moscow kumvamia jirani yake Februari 24.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *