Kitengo cha kijeshi cha Hamas kinachojulikana kama Ezzedine Al-Qassam, kilikabidhi mabaki ya mateka wawili jana Jumamosi usiku kama sehemu ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Marekani.

Ofisi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu imethibitisha kuwa Shirika la Msalaba Mwekundu lilipokea mabaki hayo na kuyakabidhi kwa wanajeshi wa nchi hiyo kwa utambulisho.

Hamas yadaiwa kupanga mashambulio dhidi ya raia wa Gaza

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema kuwa ina ripoti za kuaminika kwamba Hamas inapanga shambulio dhidi ya raia huko Gaza, na ikaonya kwamba itakuwa ukiukaji wa makubaliano hayo ya amani.

Katika taarifa, wizara hiyo imesema ikiwa Hamas itafanya shambulizi hilo, hatua zitachukuliwa kuwalinda watu wa Gaza na kudumisha uadilifu wa makubaliano hayo bila ya kutoa ufafanuzi zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *