Wakati wa meneja Jurgen Klopp, Liverpool ilijulikana kwa kupambana kuanzia mwanzo, hili liliwasaidia kupata magoli mapema na kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza walikuwa wameshamaliza kazi. Sasa hivi hilo ni kama kitu kigeni kwao.

Wakati wa mechi yao na Manchester United, washambuliaji wanapotafuta magoli mbele, wachezaji wa nafasi ya kiungo walikuwa wanakaba katikati, wengine hawakufuata timu mbele kuongeza shinikizo. Kulikuwa na nafasi nyingi za wazi.

Wachezaji hawakuwa wanaelewana. United wakawa wanawachachafya katika maeneo yao. Inaonekana rahisi kupenya kwenye safu ya ulinzi ya Liverpool kama ilivyokuwa kwenye mechi zao dhidi ya Bournemouth, Crystal Palace na Chelsea kwa namna ilivyowapa tabu vijana wa Slot.

Ili kurejea katika hali yao ya kawaida, Liverpool inatakiwa kuhakikisha mpira unakuwa kwenye maeneo ya wapinzani wao zaidi na kuhakikisha hakuna hatari katika lango lao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *