Kuanza kwa safari hizo itakuwa mara ya kwanza tangu zaidi ya miaka miwili.

Mashuhuda wameliambia Shirika la Habari la Ufaransa AFP kuwa wamesikia sauti za droni katika maeneo ya kati na kusini mwa Kahrtoum pamoja na milipuko katika eneo la uwanja wa ndege kuanzia saa kumi asubuhi hadi saa kumi na mbili.

Uwanja huo wa ndege umefungwa tangu mapigano yalipozuka Aprili 2023 kati ya jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF na kusababisha miundombinu muhimu kuharibiwa katika mji huo mkuu.

Khartoum imekuwa na utulivu tangu jeshi lilipochukua udhibiti mapema mwaka huu, ila mashambulizi ya droni yameendelea, huku wanamgambo wa RSF wakituhumiwa kuilenga miundombinu ya kijeshi na kiraia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *