
Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio baada ya kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov. Trump amethibitisha taarifa hiyo akisema haitaji kuwa na mkutano usio na tija wala kupoteza muda.
Urusi kwa upande wake imesema maandalizi ya mkutano huo kati ya Trump na Putin yanaendelea lakini kwanza kunahitajika kukubaliana katika mambo kadhaa muhimu. Ikulu ya Kremlin imetoa tangazo baadaye na kusisitiza kuwa masharti yake ili kufikia amani nchini Ukraine bado hayajabadilika.