Viongozi wa dunia, wataalam wa Afya na wanasayansi wanakutana Afrika Kusini siku chache kabla kikao cha G20,kuja  na msimamo  kuhusu  njia  za kufadhili afya bila kutegemea  ufadhili wa kigeni.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mkurugenzi wa  kituo cha kudhiibiti magonjwa  Afrika CDC dkt Jean Kaseya anasema  utegemezi huo unaweka Afrika hatarini kukiwa na ongezeko la magonjwa  ya mlipuko, akisema  hadi sasa  Afrika haipo tayari kukabiliana na magonjwa  ya majanga.

Mpango wa kwanza mbadala wa ufadhili ni ufadhili wa ndani ya nchi tofauti ,nchi ziweze kujituma zaidi kuongeza rasli mali kwa sekta ya afya. 

Aidha kikao hicho cha nne kuhusu afya ya umma CPHIA 2025 kinatazamia  kuisadia nchi za Afrika  kuja na mipango ya afya ya umma inayofanya kazi, kulingana na mwandishi wetu maalumu Korir Caroline, ambaye anahudhuria kongamano hilo la afya huko Durban, nchini Afrika Kusini.

“Afrika inakumbana na changamoto si haba,na kila kunapokuwa na majanga yanazuka Afrika tupo kwenye hatari , ukiangalia magonjwa ya milipuko yako Afrika kwa mfano, mwaka 2024 tulishuhudia ongezeko la magonjwa ya milipuko la aslimia 41,na ukiangalia mitindo ya 2024 na  2025 tulikuwa na asilimia kubwa ya MPOX,ukiangalia maambukizo ya Kipindupindu yanafanana, sasa tunaingia kipindi ambapo wanafunzi wengi watakuwa likizo,sjui Kipindupindu itakuwaje mwishoni mwa mwaka huu” , amesema dkt Jean Kaseya.

Profesa Omu Anzele kutoka chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya naye anaeleza baadhi ya ufadhili Afrika inaweza kukumbatia:

Ni serikali kwanza kisha wanafuatia wafadhili wengine,tatu, tunaweka wapi taasisi za kikanda EAC , ECOWAS na benki za Afrika. Mwishowe tuangalie ,nani wadau wapya ulimwenguni, katika ufadhili wa afya tukiachana na wale wa kihistoria ,pia Ulaya na sasa pia Asia ,hivi karibuni kumekuwa na mvuto Asia kutoa ufadhili,lakini mjue wao hawatoi ufadhili kawaida,hii ni milango ambayo mpaka tubishe wenyewe.

Kwa upande wake  Dr Shiva Murugasampilay kutoka taasisi ya afya ya umma Zimbabwe anaeleza mchango wa mifumo ya kuzuia magonjwa ya milipuko.

Sharti tubadilishe mifumo yetu,kutoka hospitali ,kutibu magonjwa hadi kuzuia magonjwa kwa kuishi maisha yenye afya,tunafanya mengi kutibu na mbinu za zima moto. Vitengo vya afya ambavyo vimeathirika na kupungua ufadhili wa kigeni ni pamoja na Malaria,HIV TB na utoaji chanjo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *