
Onyo hilo la Umoja wa Mataifa linakuja huku muda wa mwisho wa kubuniwa kwa serikali mpya ukiwa unakaribia.
Haiti bado haijatangaza tarehe ya uchaguzi mkuu ambao utakuwa wa kwanza katika kipindi cha karibu mwongo mmoja, wakati ambapo uhalifu unaofanywa na magenge ukiwa unazidi kuuzonga mji mkuu na viunga vyake.
Maandalizi ya kiufundi ya uchaguzi huo lakini yameshaanza. Baraza la muda la uchaguzi nchini Haiti limesema kuwa awamu ya kwanza ya uchaguzi huo itagharimu karibu dola milioni 140.
Wizara ya sheria ya haiti imetangaza kuwa zaidi ya vyama 220 vya kisiasa vimeanza mchakato wa kujisajili.