Mkoa wa Morogoro una mtandao wa Barabara wa kilometa 2,071.23, katika mtandao huo, Barabara kuu ni kilometa 849.43 na Barabara za mkoa ni kilometa 1,221.81.Aidha jumla ya Kilomita 510.37 za Barabara kuu ni za kiwango cha lami na kilomita 339.06 ni za changarawe, kwa Barabara za mkoa kilomita 190.32 ni za lami na kilomita 1,031.49 ni za changarawe.
Mkoa wa Morogoro umepokea kiasi cha shilingi bilioni 712 Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuhudumia miradi ya miundombinu ya Barabara Pamoja na madaraja katika mkoa wa Morogoro huku miradi 7 ya Dharula ya Ujenzi wa Madaraja (CERC) inayofadhiliwa na Benki ya Dunia yenye thamani ya Shilingi bilioni 37.840 ikiwa inaendelea kwa kasi kuboresha miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua za El-nino pamoja na Kimbunga hidaya
Hayo yamebainishwa na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro Mhandisi John Mkumbo ofisini kwake leo tarehe 25 Octoba 2025 wakati akizungumzia kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani ambaye ametoa shilingi bilioni 712 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya Barabara na madaraja.
Mhandisi Mkumbo ameitaja miradi hiyo kuwa ni Pamoja na Ujenzi Daraja la Chakwale katika Barabara ya Iyogwe – Chakwale – Ngiloli unaojengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.438, Ujenzi Daraja la Nguyami Barabara ya Iyogwe – Chakwale – Ngiloli kwa gharama ya shilingi Bilioni 7.166, Ujenzi Daraja la Kihonda katika Barabara kuu ya Morogoro – Dodoma kwa gharama ya shilingi bilioni 5.311, Ujenzi Daraja la Bwage katika barabara Mziha – Turiani na Daraja la Mjonga barabara ya Mvomero – Ndole Kibati kwa gharama ya shilingi bilioni 10.038, Ujenzi Daraja la Doma katika Barabara kuu ya Tanzam kwa gharama ya shilingi bilioni 4.146 na Ujenzi Daraja la Ngerengere katika Barabara kuu ya Morogoro – Dodoma kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.737
#StarTvUpdate
