Na sasa kesi yake iko mbele ya mahakama, huku akiwakilishwa na wakili aliyeteuliwa na mahakama.
ICC inadai kumshtaki kwa makosa 39 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, yakiwemo mauaji, ubakaji, kutumia watoto kama wanajeshi, na utumwa wa jinsia, kati ya 2002 na 2005.
Kamanda mwengine wa LRA, Dominic Ongwen, alihukumiwa na ICC mwaka 2020 kwa makosa 61 yanayofanana na yale ya Kony.
Ongwen mwenyewe alitekwa nyara na wanamgambo akiwa kijana wa miaka 9, akabadilishwa na kuwa mwanajeshi mtoto na baadaye kuwa kamanda katika kundi hilo la waasi.
Kwa sasa Ongwen anatumikia kifungo chake cha miaka 25 nchini Norway.
Wakati kesi ya Joseph Kony inaposikilizwa waathirika bado wanasubiri kwa hamu kuona hukumu itakayotolewa.
Lakini raia wengine wa Uganda wanadai kuwa kuanza kesi ya Kony bila yeye mwenyewe kuwepo au bila kujua hata kama ako hai haina uzitoi kwani hata akipatikana kuwa na hatia haki haitatendeka ikiwa hatakamatwa.