s

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ripoti zinasema, nyumba na maduka kuzunguka Kanisa huko Komanda yalishambuliwa vibaya na waasi.

    • Author, Yusuph Mazimu
    • Nafasi,

Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa sasa ni uwanja wa mateso, hofu, na umwagaji damu unaoendelea bila kikomo.

Katika mazingira ya mizozo ya muda mrefu, vikundi vya waasi wenye silaha kama ADF (Allied Democratic Forces) na M23, vinahusishwa moja kwa moja na mauaji ya halaiki, hasa dhidi ya Wakristo.

Kwa mujibu wa taarifa ya hivi karibuni ya Bunge la Ulaya (3 Aprili 2025), wakristo wamekuwa wakilengwa kwa makusudi kwa kushambuliwa, kuuawa, kutekwa na makanisa yao kuvunjwa au kuchomwa moto.

Usiku wa Jumapili ya Julai 27, 2025, wakristo 43 waliokusanyika katika ibada ya usiku katika kanisa katoliki lililoko Komanda, mkoa wa Ituri Mashariki mwa DRC. Wakiwa katika maombi ya amani, waumini hao waliuawa kikatili kwa risasi, mapanga na kuchomwa moto na waasi wa kundi la ADF linalohusishwa na ISIS.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *