s

    • Author, Florian Kaijage
    • Nafasi,

Julai 13, 2025 aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchni Cuba, Humphrey Polepole alitangaa kujiuzulu nafasi hiyo na nafasi nyingine za utumishi umma Jumapili akitaja sababu kadhaa za kufikia uamuzi huo ambao haukutarajiwa na wengi.

Sababu kuu alizotaja ni ukiukwaji wa taratibu za chama cha CCM, kupinga matendo ya utekaji wa watu na utendaji wa serikali. Yote hayo aliyafafanua kwa kina siku tano baadaye Ijumaa Julai 18, 2025 wakati wa taarifa mubashara kupitia mtandao wa Facebook.

Na ameendelea kuelezea anachoamini kuwa ‘mambo kwenda mrama’ kwenye chama, alipohojiwa na mwanahabari mkongwe na mwanasheria aliyewahi kushika nyadhifa kadhaa serikalini, Jenerali Twaha Ulimwengu.

Ushahidi wa uamuzi na tangazo la kujiuzulu kwa Polepole kuwashtua watu wengi ni machapisho kwenye mitandao ya kijamii kuelezea kuwa tangazo lililokuwa kwenye barua ya Polepole kwenda kwa Mwenyekiti wa chama chake na Rais wa nchi Samia Suluhu Hassan halikuwa la kweli, kiasi kwamba Polepole mwenyewe aliamua kuwajibu moja kwa moja mitandaoni kuwa barua ile ilikuwa ni ya kwake.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *