Nchini Colombia, mapigano na mivutano na makundi yaliyojitenga ya FARC yanaendelea. Siku ya Jumanne, Agosti 26, Waziri wa Ulinzi amethibitisha kwamba wanajeshi 34 wamechukuliwa mateka katika eneo la Guaviare, kusini mwa nchi hiyo. Raia wanaotumiwa na kundi la waasi la FARC wanaaminika kuhusika na shambulio hilo. Colombia inakabiliwa na mzozo mbaya zaidi wa ghasia kwa kipindi cha muongo mmoja.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu nchini Colombia, Najet Benrabaa

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Waziri wa Ulinzi wa Colombia Pedro Sanchez amezungumzia “hatua isiyo halali, ya uhalifu ya baadhi ya watu waliovaa nguo za kiraia wanaodai kuwashikilia askari.” Kwake, ni wazi kuwa raia wanatumiwa, kwani wanaomba, badala ya kuachiliwa kwa mateka, kurejeshwa kwa miili ya wapinzani wa FARC (Jeshi la Mapinduzi la Colombia) wa jimbo la Guaviare, wanachama wa EMC (makao makuu wapiganaji hao).

Nchini Colombia, makundi yenye silaha mara nyingi hutumia vitendo hivi, kwa kuzingatia ukweli kwamba vikosi vya usalama havishambulii raia. Vile vile, utekaji nyara hutokea mara nyingi, lakini mara chache watu wengi huchukuliwa mateka.

Kuongezeka kwa vitendo vya utekaji nyara

Hii inadhihirisha wazi ongezeko la mivutano na ghasia nchini. Tangu wiki iliyopita, jeshi limezidisha hatua zake dhidi ya kundi hili lililojitenga na FARC, ambalo lilitekeleza shambulio la bomu lililotegwa katika lori ambalo liliua watu sita na kujeruhi 60 huko Cali mnamo Agosti 22. Siku hiyo, karibu na Medellin, jiji la pili kwa ukubwa nchini, maafisa wa polisi 13 waliuawa katika ufyatulianaji wa risasi na kundi la watu wenye silaha. Mamlaka ilihusisha shambulio hilo na kundi dogo la EMC, lililo katika mzozo na tawi lake kuu linaloongozwa na Ivan Mordisco.

Baada ya mashambulio haya, Waziri wa Ulinzi alihakikisha kwamba serikali ya Colombia ilikuwa ikitumia njia zote “kuondoa vitisho” kwa usalama. Mapigano yalisababisha wapiganaji kumi wa kundi lililojitenga na FARC kuuawa na wawili kukamatwa. Kwa upande wake, kiongozi wa EMC kundi la wapiganaji waliojitenga na FARC, Ivan Mordisco, amekosoa mpango wa amani wa serikali, na kuuita “mkakati wa vita.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *