S

Chanzo cha picha, URT/SALUM

Tume huru ya Taifa ya uchaguzi nchini Tanzania (INEC) imeteua rasmi majina ya wagombea 17 wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Hatua hii imekuja baada ya wagombea hao kutoka vyama 17 kurejesha fomu na kukidhi masharti ya kikatiba na kisheria.

CHADEMA, chama kikuu cha upinzani, hakitashiriki uchaguzi huu kikisisitiza kuwa marekebisho ya mfumo wa uchaguzi ni sharti yafanyike kwanza ili kuwe na uchaguzi huru na wa haki.

ACT-Wazalendo pia haitakuwa na mgombea baada ya Luhaga Mpina kuenguliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kufuatia pingamizi lililotolewa na mwanachama wa chama hicho, Monalisa Ndala.

Sababu kuu iliyoelezwa ni kwamba Mpina alipata uanachama Agosti 5, 2025, nje ya muda wa kisheria wa kuchukua fomu za kugombea ndani ya chama, ambapo ilipaswa kuwa kabla ya Mei 25, 2025.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *