.

Chanzo cha picha, EPA-EFE/REX/Shutterstock

Maelezo ya picha, Waziri wa masuala ya Kigeni nchini Iran Abbas Araqchi

Katika kukabiliana na kutimuliwa kwa balozi wa nchi hiyo kutoka Australia, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imeutaja uamuzi huo kuwa “usio halali na ni kinyume na utamaduni wa uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili” huku ikisisitiza kwamba “inahifadhi haki yake ya kuchukua hatua za maelewano, huku ikiutaka upande wa Australia kufikiria upya uamuzi huo usio na msingi.”

Serikali ya Australia mnamo Jumanne (Agosti 26) iliishutumu Iran kwa kuongoza angalau mashambulizi mawili ya chuki dhidi ya Wayahudi katika ardhi yake na kutangaza kwamba itamfukuza balozi wa Iran.

Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese anasema shirika la upelelezi la serikali ya nchi hiyo limekusanya taarifa “za kuaminika” zinazoonyesha kuwa serikali ya Iran ilihusika katika “kuelekeza angalau mashambulizi mawili dhidi ya Wayahudi” nchini mwake.

Serikali ya Australia imemtaja Balozi wa Iran Ahmad Sadeghi kuwa “asiyefaa” na kumpa yeye na wanadiplomasia wengine watatu siku saba kuondoka nchini humo.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *