Alejandro Garnacho

Chanzo cha picha, getty

Maelezo ya picha, Alejandro Garnacho

Manchester United wako karibu kufikia makubaliano ya dau kati ya pauni milioni 35 na 40 kumuuza winga wa Argentina mwenye umri wa miaka 21 Alejandro Garnacho kwenda Chelsea ya Ligi Kuu England (Telegraph)

AC Milan wameingia katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Christopher Nkunku huku mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 27 pia akiwaniwa na Bayern Munich mabingwa wa Bundesliga na klabu yake ya zamani RB Leipzig (Athletic)

Newcastle wanatarajiwa kuwasilisha ofa mpya ya pauni milioni 60 kwa mshambuliaji wa Norway mwenye miaka 25 Jorgen Strand Larsen baada ya awali Wolves kukataa madau mawili ya pauni milioni 50 na 55 awali (Sky Sports)

Kipa wa Paris St-Germain Gianluigi Donnarumma bado hajaondoa matumaini ya kuondoka kabla ya dirisha kufungwa huku Manchester City ikionekana kuwa chaguo bora zaidi endapo kipa wa Brazil Ederson ataondoka klabuni hapo (Sky Sports)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *