S

Chanzo cha picha, CCM

Katika siasa za Chama Cha Mapinduzi (CCM), mojawapo ya maswali ambayo mgombea mwenza wa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano hutakiwa kujibu ni moja; ni lipi hasa analileta mezani?

Kwamba zaidi ya umaarufu wa chama, ni sifa zipi za mgombea mwenza zitaongeza nguvu ya ushawishi, kura na haiba ya mgombea wa urais? Kujibu swali hili, inabidi turudi nyuma kidogo.

Katika mazungumzo yangu na baadhi ya makada wakongwe wa CCM, wakati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, na wenzake wakiwaza kuhusu nafasi ya mgombea urais na mgombea mwenza, mambo kadhaa yalikuwa vichwani mwao.

Mosi ni kuwa utaratibu wa kupokezana urais kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar na kupunguza vita vya kuwania urais ndani ya chama. Kwa maana hiyo, wakati Dkt. Omar Ali Juma akiteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Benjamin Mkapa mwaka 1995, ilifikiriwa kuwa angekuwa mrithi wake mwaka 2005.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *