s

Chanzo cha picha, Global Publishers

    • Author, Na Sammy Awami
    • Nafasi,

Agosti 29, 2025 Mahakama kuu kanda ya Manyara imefuta amri ya Msajili wa Vyama Vya Siasa ya kuzuia ruzuku ya Chadema na kutowatambua Katibu Mkuu, Manaibu wake na wajumbe watano wa kamati kuu waliothibitishwa na Baraza kuu Januari 22, 2025 baada ya uchaguzi mkuu wa ndani ya Chama, chini ya uongozi mpya wa Mwenyekiti wake Taifa, Tundu Lissu.

Uamuzi huu unafuatia hatua ya Msajili aliyochukua mwezi Mei mwaka huu kutangaza kutengua na kutoutambua Sekretarieti ya uongozi wa chama hicho na kusitisha kutoa ruzuku kwa chama cha Chadema kwa madai ya kwamba kikako kilichowaidhinisha hakikuwa na akidi halali na inayotakiwa ambayo ni zaidi ya asilimia 50% ya wajumbe. Chadema walipingia hili Mahakamani maamuzi haya Msajili kama ambavyo ACT Wazalendo nao wako Mahakamani sasa kupinga uamuzi mwingine wenye nguvu uliofanywa na Msajili.

Kwa upande ACT Wazalendo pigo walilolipata kwa mgombea wao wa urais, Luhaga Mpina kuwekewa kizingiti na Msajili wa Vyama vya Siasa na Tume Huru ya Uchaguzi kutomteua itakuwa imewakumbusha kesi waliyoshiriki kuifungua miaka kadhaa iliyopita wakipinga Sheria ya Vyama vya Siasa. Yanayotokea sasa, yanaleta mjadala kuhusu nguvu kubwa na mamlaka ya Msajili wa vyama vya siasa.

Wasiwasi wa Chadema, ACT Wazalendo na Wanaharakati

Maamuzi makubwa kama haya ya kutengua uongozi wa vyama, kuzuia wagombea kutogombea yanayofanywa na ofisi ya Msajili ndio yaliibua wasiwasi mwaka 2019, na kuwasukuma Wenyeviti wa zamani wa ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, CHADEMA, Freeman Mbowe, CHAUMMA, Hashim Rungwe, Kiongozi wa wakati ule wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe, na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA wa wakati ule Salum Mwalim kufungua kesi kwa niaba ya vyama vingine 10 katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *