.

Kikao cha kamati ya uongozi wa chama cha ACT Wazalendo nchini Tanzania kimemvua uanachama Monalisa Joseph Ndala, kufuatia hatua yake ya kuwasilisha malalamiko kwa msajili wa vyama vya siasa yaliyosababisha Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) kumuengua mgombea wa urais wa chama hicho.

Luhaga Mpina aliyeteuliwa na Chama cha ACT – Wazalendo kuwania urais alienguliwa na INEC kufuatia uamuzi wa ya Msajili wa Vyama vya Siasa kukubaliana na hoja za Monalisa.

Sababu kuu iliyoelezwa na Monalisa ni kwamba Mpina alipata uanachama Agosti 5, 2025, nje ya muda wa kisheria wa kuchukua fomu za kugombea ndani ya chama, ambapo ilipaswa kuwa kabla ya Mei 25, 2025.

Taarifa iliyotiwa saini na kutumwa katika vyombo vya habari na katibu wa tawi la Mafifi mkoani Iringa, Neema Ernest Kivamba, imeeleza kuwa mkutano uliofanyika katika tawi hilo vilevile ulibaini kwamba Monalisa ameshindwa kutekeleza matakwa ya katiba ya chama hivyo basi kupoteza sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha ACT – Wazalendo.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *