Akanji

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Akanji

Tottenham Hotspur wanaongoza mbio za kumsajili beki wa Manchester City Manuel Akanji, mwenye umri wa miaka 30, wakilenga kuwazidi ujanja AC Milan na Crystal Palace kupata sahihi yake. (Gazetta Dello Sport)

Kocha mkuu wa Barcelona Hansi Flick amesema anaamini kuwa kiungo mshambuliaji mwenye umri wa miaka 22 Fermin Lopez, ambaye ameichezea Hispania mara mbili, hataondoka klabuni hapo katika dirisha hili la usajili licha ya kuhusishwa na Chelsea. (ESPN)

Lakini Chelsea wako tayari kutoa ofa nono kwa ajili ya Lopez, ambaye thamani yake Barcelona ni euro milioni 90 (£78m). (Mundo Deportivo)

West Ham wameingia katika mbio za kumsajili Fabio Vieira kutoka Arsenal, lakini Stuttgart na klabu nyingine kubwa ya Bundesliga pia wanavutiwa na kiungo huyo Mreno mwenye umri wa miaka 25. (Sky Sports Germany)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *