Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Anicet-Georges Dologuele, ameamua kufuta uraia wake wa Ufaransa, ili kuwania urais katika nchi yake.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Hatua hii inamaanisha kuwa, anajiandaa kumenyana na rais wa sasa Faustin Touadera, wakati uchaguzi huo utakapofanyika Desemba tarehe 28 mwaka huu.

Mwanasiasa huyo wa upinzani amesema, uamuzi aliuchukua ni binafsi, na kuitaka Tume ya uchaguzi kuhakikisha kuwa, uchaguzi huo unakuwa huru na haki.

Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa   Dologuele, kujaribu kutafuta uongozi wa nchi hiyo. Mwaka 2020 aliwania, na kumaliza katika nafasi ya pili, katika uchaguzi ambao ulidaiwa kugubikwa na wizi wa kura.

Wachambuzi wa siasa wanasema, hatua hii ya mwanasiasa huyo maarufu imesukumwa na kile ambacho wapinzani wa  Touadera wanasema, unatokana na mpango wa kiongozi huyo  kuwa na mpango wa kusalia madarakani kwa muda mrefu, baada ya kubadilisha katiba mwaka 2023 ili awanie muhula wa tatu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *